USHINDE UTUMWA KIZUIZI CHA MAFANIKIO YAKO
Ili usonge mbele na ufikie malengo ya maisha yako ni lazima UUSHINDE UTUMWA unaokuwekea mipaka. Kuna watu ambao wanataka kuendelea kuwa karibu na wewe na uwe chini ya HIMAYA yao... ...sio kwa sababu WANAKUPENDA bali kwa sababu umekuwa mtumwa wao. Mwandishi maarufu wa Marekani, Fredrick Douglas (1118-1895) aliwahi kusema... ...“Sikuwahi kujua kuwa mimi ni MTUMWA hadi pale nilipogundua kuwa siwezi kufanya yale NILIYOYATAKA”. Kuna utumwa wa KIHISIA, mtu hakupi nafasi ya kufurahia unachotaka... ...na kila siku anakuumiza na hauna pa kwenda wala hauna cha kumfanya. Hataki uhusiane na wengine zaidi yake. Kuna utumwa wa KIAKILI, mtu hataki utumie mawazo yako... ...anataka anachosema yeye ndio kiongoze maisha yako, hutakiwi kubisha. Kuna utumwa wa KIUCHUMI, mtu anatengeneza mazingira UMTEGEMEE maisha yako yote na usiwe na uhuru wako wa kifedha. Kuna utumwa wa KIROHO, anatumia nguvu za kiroho kuteka AKILI yako na anakuendesha ufanye anavyotaka yeye. Ukigundua uko kwenye aina yoyote ya utum...